Unapookoka neno la mungu huanza kushughulikia akili zako
Unapookoka neno la mungu huanza kushughulikia akili zako

Unapookoka neno la mungu huanza kushughulikia akili zako

𝐾𝑖𝑑𝑎 𝐼𝑏𝑟𝑎ℎ𝑖𝑚✪

10 min174 plays
Comedy & Entertainment
Play

Description

<p>1 Petro 2:1-2<br /> “Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote. Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu;”</p> <p>Hakusema maziwa ya Roho amesema maziwa ya akili, Neno la Mungu unalopewa unapookoka mahali pa kushughulika napo pa kwanza ni akili zako ili upate kuukulia wokovu, ndio maana akili zikibanwa haijalishi umeokoka miaka mingapi huwezi kukua kiroho, ndio maana huwezi kujivunia miaka uliyokaa ndani ya wokovu, Mungu anaangalia umekua kiasi gani na usipojua kwamba Mungu kaziweka akili kwa makusudi kabisa macho na ubongo vitakusaidia kusoma Biblia lakini haviwezi vikakusaidia kuelewa.</p> <p>Mathayo 7:24<br /> “Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba. Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga; mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.”</p> <p>Huyu ni Yesu anazungumza anasema mtendaji wa Neno amefaninishwa na mtu mwenye akili hajasema amefananishwa na wa kiroho.</p> <p>Watu wengi sana hawajui namna ya kuunganisha akili na imani, wanafikiri mtu aliyeokoka akitumia akili anaenda kimwili na sasa umeelewa kwamba akili haziko kwenye mwili, Biblia imekataza tusizitegemee akili lakini tuzitumie akili.</p> <p>Yule mtu ambaye alikuwa na kichaa alipofunguliwa yale mapepo wale watu kwenye kijiji walikuja kumtazama pamoja nakumwona amevaa nguo na ana utulivu wakagundua ana akili zake. Maana yake walitambua ya kwamba huyu mtu maisha aliyokuwa anaishi akili hazikuwa kazini.</p> <p>Ukisoma hiyo mistari vizuri kwa jicho la mwalimu kuna kitu hapo utaona<br /> Luka 8:22,37<br /> “Ikawa siku zile mojawapo alipanda chomboni yeye na wanafunzi wake, akawaambia, Na tuv

Uploader

daisy.road

daisy.road

Unapookoka neno la mungu huanza kushughulikia akili zako - Listen Free | WowFM