Namna ya kujiandaa kukikabili kipindi hiki cha siku za mwisho (Sehemu ya tatu)
Namna ya kujiandaa kukikabili kipindi hiki cha siku za mwisho (Sehemu ya tatu)

Namna ya kujiandaa kukikabili kipindi hiki cha siku za mwisho (Sehemu ya tatu)

𝐾𝑖𝑑𝑎 𝐼𝑏𝑟𝑎ℎ𝑖𝑚✪

10 min174 plays
Comedy & Entertainment
Play

Description

<p>Tutakusanyika mbele za Bwana tutaimba na kushangilia. Kama Yesu asingekufa msalabani safari yake ingekuwa bure. Maana angeishia kuponya watu na ingekuwa bure tu. Kama asingekufa na akafufuka ingekuwa shida sana. Biblia inasema ulitokea ubishi juu ya kiama ya wafu ule ubishi ulileta mtengano katika dini ya wayahudi na ukatengeneza dini ya masadukayo. Ugomvi wao ulikuwa ni imani yao juu ya kiama ya wafu. Huo ubishi ukaletea mgawanyo mpaka ndani ya kanisa wakati ambao watu wameanza kuokoka.</p> <p>Ilibidi Roho Mtakatifu amsemeshe Paulo aandike barua kwa Wakorintho ili wajue kuwa kama Kristo hakufufuka imani yetu ni bure maana yake haina faida. Kama Kristo hakufufuka tumekuwa masikini kuliko watu wote ambao tunamtegemea Bwana. Kama Kristo amefufuka tunajua na sisi kwamba atatufufua. Kwa sababu hiyo anasema ni tumaini lenye baraka kama ambavyo Tito alivyoandika.</p> <p>Endelea kuimba wimbo huo “Wateule wote tutakusanyika”</p> <p>Wimbo huu ukuandae kufanya sala ya toba. Kama uliokoka ukarudi nyuma rudi tena kwa Mungu. Pia kama unajua kabisa Yesu akija leo huna uhakika kama utaenda nae rudi kwa Bwana.</p> <p>Siku moja nilikuwa kwenye ndege mimi na Rubani mmoja. Tulikuwa wawili tu. Akaniambia akipata shida je ntafanyeje. Basi akaanza kunionesha namna ya kushika usukani wa ndege na namna ya kuendesha ndege. Akanionesha mpaka namna ya kutumia breki za ndege. Sasa nikatazama chini, niliona kulivyo mbali sana. Pia nikaona namna tunavyopita mawinguni. Ghafla nikakumbuka “mstari kuwa tutakusanyika kumlaki Bwana Mungu mawinguni”. Yule Rubani alikuwa kaokoka Nikamwambia kuwa ikipigwa tarumbeta ya kuondoka na Yesu akija hapa kutunyakua tutaenda naye na hii ndege itajijua itakakoenda. Lakini kama Mungu anataka tubaki tutabaki.</p> <p>Ni hatari sana kukaa dakika moja mahali na hujui kama Yesu akitokea hapa utaenda naye. Ni hatari sana kwa sababu Yesu yupo, hata kama huamini kama Yupo. Wainjilisti huwa wanatuambia kuwa kama utaamini Yesu yupo hutakuwa na hasara kama usipomkuta ila utakuwa na hasara sana kama utaamini hayup

Uploader

daisy.road

daisy.road

Namna ya kujiandaa kukikabili kipindi hiki cha siku za mwisho (Sehemu ya tatu) - Listen Free | WowFM