Kumwamini Mungu kwa kumfuata Yesu Kristo (Sehemu ya Nne)
Kumwamini Mungu kwa kumfuata Yesu Kristo (Sehemu ya Nne)

Kumwamini Mungu kwa kumfuata Yesu Kristo (Sehemu ya Nne)

๐พ๐‘–๐‘‘๐‘Ž ๐ผ๐‘๐‘Ÿ๐‘Žโ„Ž๐‘–๐‘šโœช

9 min
Comedy & Entertainment
Play

Description

<p>Tunapozungumza juu ya kumtumikia Mungu watu wengi sana hufikiria watu wachache tu yaani wahubiri, wachungaji, wainjilisti au wanaofanya kazi kanisani. Lakini kwenye Biblia inasema kila kiungo katika mwili wa Kristo kina nafasi yake na kazi yake kwa hiyo ni mtumishi wa Mungu. Inawezekana usihubiri, lakini pale ulipo ni mtumishi wa Mungu maana yake usimame katika kusudi lake ni kueneza Ufalme wake katika kazi ufanyayo. Hakikisha watu wanamjua Mungu maana Biblia inasema kila aliye mwana anao ushuhuda haisemi kila aliye mtumishi.</p> <p>Lakini pia kuna watu wengine ambao wanamtumikia Mungu bila wao kujua hata Israeli aliambiwa nimekufunga mshipi ingawa hukunijua ili wapate kunijua mimi ya kwamba hakuna Mungu kama mimi Kwa hiyo wakati Mungu anamchukua Israeli ili amtumie Israeli kujifunua kwa ulimwengu, Mungu anasema Israeli hakumjua. Kwa hiyo Mungu anaweza kukutumia wakati wewe humjui kwa sababu zake yeye, anaweza kujifunua wakati anaendelea kukutumia au anaweza kunyamaza.</p> <p>Maana Yesu anasema Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, kwa hiyo kwenye jambo lolote la kumtumikia Mungu, kwenye jambo lolote la kuishi hapa duniani, kati ya lengo mojawapo ambalo Mungu anategemea kila mtu awe nalo liwe ni lengo la kukutana na Yesu na kuishi naye milele Hivyo ni muhimu sana kuzungumza na waliokuzunguka kwa habari ya maisha yao na Yesu kabla ya kuondoka hapa duniani ndivyo Wathesalonike inavyotuambia</p> <p>1 Wathesalonike 4:13-16<br /> โ€œLakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini. Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye. Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti. Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.โ€</p> <p

Uploader

daisy.road

daisy.road

Kumwamini Mungu kwa kumfuata Yesu Kristo (Sehemu ya Nne) - Listen Free | WowFM